Wednesday, May 14, 2008

Miss Tanga 2008 lapata Wadhamini Wapya

Kampuni ya Tanga Fresh yaipiga tafu Miss Tanga 2008

MCHUANO wa kumsaka Kisura wa Tanga ndio kama hivyo umekwishaanza kutimua vumbi lake, huku kampuni mbalimbali zikithibitisha udhamini wao. Kampuni ya Maziwa ya Tanga Fresh Limited nayo imetangaza udhamini mnono.

Meneja Mwandamizi wa kampuni hiyo Alnoor Hussein inayozalisha aina mbalimbali za maziwa, maziwa ya mgando na jibini alisema kampuni yao imejikita kudhamini mashindano hayo ikiwa ni mkakati wa kampuni yake kuzitangaza bidhaa zake kupitia mashindano kama haya katika kuhimiza matumizi ya maziwa kama njia ya kuboresha afya na nguvu katika miili na pia kuipa sapoti michuano hiyo.

Alnoor aliwataka wadhamini wengine wajitokeze ili kudhamini mashindano hayo ili kuboresha zaidi akisema kuwa mashindano kama haya yanatoa ajira kwa wasichana ikiwa ni pamoja na kuboresha maisha yao na kuwajengea kujiamini.
Alisema pamoja na udhamini huo, warembo watapapewa bidhaa zake kwa ajili ya kuimarisha ngozi zao pamoja na kupata fursa ya kufanya ziara katika kiwanda hicho bora cha maziwa nchini ili kuona jinsi wanavyoendesha shughuli zao.


Hoteli mpya na ya Kisasa Tanga. Inasemekana ni Hotel pekee mjini Tanga ambayo itakuwa inatumia kadi kufungua milango. Regal Naivera Hotel wamejitokeza kudhamini miss Tanga 2008.









KARATA CLASSIC FURNITURE
"Where Confrotability & Durability meet?"

Kampuni ya Karata classic furniture iliyoko maeneo ya Taifa Road, Mkabala na Mabanda ya Papa kwenye kona ya kuingia soko la Mgandini jijini Tanga ni moja ya wadhamni wa Miss Tanga 2008.


Kampuni hii bingwa wa furniture wanatengeneza kila aina ya sofa, vitanda, na meza za chakula, yaani furniture zote za living Room, Dinning Room, Bed Room na Ofisini kwa dizaini ya kisasa na zilizotengenezwa kwa ubora wa hali ya juu na za uhakika zaidi.


Karata Classic Furniture ni suluhisho la thamani za majumbani na ofisini pia.


Kwa mahitaji yako wasiliana nao kwa: 0754 148 169 na 0717 906 567 au kwa barua pepe: karatafurniture@gmail.com

Wednesday, April 30, 2008

Mchaka mchaka Miss Tanga Umeanza

MISS VYUO NAO HAO....
Jumla ya Warembo 10 wamejitokeza kuwania nafasi za kujikita Miss Tanga kupitia taji la Miss Collage. Watano kati ya hao wataingia moja kwa moja kambi ya miss Tanga wakiwa na wenzao kutoka miss Usagara, Miss Korogwe na Miss Lushoto. Taji la Miss Collage mpaka sasa limeshikiliwa na Victoria Martin ambaye pia ni Miss Tanga, Miss Kanda ya Kaskazini na Balozi wa Redds 2007.
Mwaka jana ilikuwa hivi: Mratibu wa shindano la Miss College 2008, Maximilian Luhanga ambaye pia ni Mkurugenzi wa New Face Entertenment iliyopewa dhamana ya kuandaa kitogoji hicho alisema onyesho litafanyika Habours Club jijini Tanga. Miss collage 2008 limedhaminiwa na Redds, Mwananchi Communication, Golden Pulm Café, Sofia Records na Mwambao FM.

Wanaochuana kuwania taji hilo ni Mariam Hajibu, Beatrice Liwemba, Evelyne Balozi, Mwajuma Msangi, Mariam Mhando, Silvia Urio, Dorice Steven, Mwanamina Bausi, Halima Khalfan na Agnes Mwakipesile, kama wanavyoonekana pichani chini.

Mshindi wa kwanza atajinyakulia seti ya Televisen, wa pili na wa tatu watapewa simu za mkononi wakati watakaoshika nafasi ya nne hadi 10 watapata fursa ya kufunguliwa akaunti katika benki ya Backleys Jijini hapa.

Na mshindi ni...!



MISS USAGARA JUKWAANI...
MBIO za kumsaka mrembo wa Tanga zimeanza! Jumla ya warembo 9 walipanda jukwaani kuchuana kuwania nafasi za kushiriki katika shindano la Miss Tanga kupitia kitogoji cha Miss Usagara, ambapo tano bora ya warembo hao watapata tiketi ya moja kwa moja kuingia katika fainali za Miss Tanga 2008.

Kitongoji hicho cha kwanza kufanyika Miss Usagara 2008, kimefanyika Mei 2 katika Ukumbi wa Splended Jijini hapa, ambapo mwanamuziki wa muziki wa kizazi kipya nchini anayetamba kwa sasa na wimbo wake Ni Soo!, Haji Mtepa al'maarufu kwa jina la Pasha ndiye aliyetifua vumbi usiku huo katika kinyang'anyiro hicho.

Onyesho hilo linaratibiwa na Lilian Kihama Maim kupitia kampuni yake ya Sunrise Secretarial & Beauty Saloon na limefanyika katika Ukumbi wa Splended Jijini hapa.
Warembo hao tisa walikuwa ni pamoja na Aisha Abdallah, Judith Asei, Hawa Njama, Amina Sadik, Khadija Ramadhani, Salma Mohamed, Merry Fedrick, Oliva Mango na Nuru Sheshe.

Judith Assey ndiye aliyetwaa taji la Miss Usagara 2008.

Mshindi wa pili kulia ni Oliver Mango na mshindi wa tatu kushoto ni Nuru Salim. Aliyevikwa taji la Mwenye kipaji kwa warembo wa Usagara ni Amina Sadick na taji la tabia njema lilikwenda kwa Hadija Ramadhani Kulia. Tano bora ya miss usagara inaingia moja kwa moja katika fainali za Miss Tanga 2008.

MIss Lushoto nayo hiyo..

Wednesday, April 23, 2008

Beauty with Purpose



Baada ya kuvikwa mataji ya Miss Tanga, Dollywood Miss Photogenic, Miss Kanda ya Kaskazini, Miss Redds Fashion Ambassador Victoria Martin hivi karibuni alichaguliwa pia kukampeni dhidi ya ugonjwa wa saratani ya matiti kwa wanawake na chama cha wanawake waathirika wa ugonjwa wa saratani ya matiti Tanzania. chama hicho kina lenga kusaidia wanawake wenzao kwa kuwapa mawaidha na kuwasaidia kwa matibabu ambayo yanasemekana kuwa ya ghali na kuwapatia matiti bandia n.k. Kama unataka kusaidia piga simu namba 0713 711413 tutakuunganisha. Pichani ni Victoria akitoa misaada kwa wanawake walioathirika na ugonjwa wa kansa (Saratani) katika siku ya wapendanao duniani, kama namna ya kuonyesha ishara ya upendo.

Breaking The Good News...


Miss Tanga2007, Miss Tanzania Kanda ya Kaskazini, Redds fashion Ambassador Victoria Martin akiongea na mwandishi wa habari kuhusu mikataba yake na kampuni za Modelling za South Afika. Vicky hivi karibuni alikwenda South Afica kuangalia soko la uanamitindo na tayari kampuni mbili zimevutiwa naye na kumpa mapendekezo yao. Kampuni hizo ni O Model na EXTRA.

Mshindi wa shindano la Big Bro Africa II 2007 Tatiana Durao akiwa amepozi na balozi wa Redds Victoria Martin leo asubuhi ndani ya hoteli ya Movenpick baada ya kuwasili kwa ajili ya kuongea na waandishi wa habari kuhusu maonyesho ya mavazi nchini.


Hapa wanafurahia jambo



Vicky ampokea Tatiana


Mshindi wa tatu wa shindano la Big Brother Africa II mwaka 2007 Tatiana Durao akiwa airport baada ya kupokelewa na balozi wa Redds, Miss Tanga 2007, Miss Tanzania Kanda ya Kaskazini Victoria Martin baada ya kuwasili katika uwanja wa ndege wa kimataifa wa Mwalimu Julius K. Nyerere jana kwa ajili ya maonyesho mawili ya mavazi. Guess who? amepagwa kuchill naye akiwa bongo.... Vicky.

KAZI ZA KIJAMII

PONGEZI:
Victoria Martin akiwapongoza wakina mama waliojifungua siku ya mkesha wa siku ya wanawake duniani ambayo huadhimishwa kila tarehe 8 March





Nasi mkuu wa Hospitali ya Agakhan akishukuru mbele ya vyombo vya habari kwa kutembelewa hospitalini hapo na kwa zawadi.


MSAADA:

Victoria na wengine na Watoto yatima wa Tanzania Mitindo House


Miss Tanga, Balozi wa Redds Victoria Martin akimkabidhi mgeni rasmi Mama Anna Kilango kiasi cha shilingi laki mbili cash ikiwa ni moja ya mchango wake katika kukizindia kituo cha watoto yatima cha (Tanzania Mitindo House) kilichoasisiwa na Khadija Mwanamboka na wenzake.