Wednesday, April 23, 2008

Beauty with Purpose



Baada ya kuvikwa mataji ya Miss Tanga, Dollywood Miss Photogenic, Miss Kanda ya Kaskazini, Miss Redds Fashion Ambassador Victoria Martin hivi karibuni alichaguliwa pia kukampeni dhidi ya ugonjwa wa saratani ya matiti kwa wanawake na chama cha wanawake waathirika wa ugonjwa wa saratani ya matiti Tanzania. chama hicho kina lenga kusaidia wanawake wenzao kwa kuwapa mawaidha na kuwasaidia kwa matibabu ambayo yanasemekana kuwa ya ghali na kuwapatia matiti bandia n.k. Kama unataka kusaidia piga simu namba 0713 711413 tutakuunganisha. Pichani ni Victoria akitoa misaada kwa wanawake walioathirika na ugonjwa wa kansa (Saratani) katika siku ya wapendanao duniani, kama namna ya kuonyesha ishara ya upendo.

No comments: