Jumla ya Warembo 10 wamejitokeza kuwania nafasi za kujikita Miss Tanga kupitia taji la Miss Collage. Watano kati ya hao wataingia moja kwa moja kambi ya miss Tanga wakiwa na wenzao kutoka miss Usagara, Miss Korogwe na Miss Lushoto. Taji la Miss Collage mpaka sasa limeshikiliwa na Victoria Martin ambaye pia ni Miss Tanga, Miss Kanda ya Kaskazini na Balozi wa Redds 2007.
Mwaka jana ilikuwa hivi:

Wanaochuana kuwania taji hilo ni Mariam Hajibu, Beatrice Liwemba, Evelyne Balozi, Mwajuma Msangi, Mariam Mhando, Silvia Urio, Dorice Steven, Mwanamina Bausi, Halima Khalfan na Agnes Mwakipesile, kama wanavyoonekana pichani chini.

Na mshindi ni...!
MISS USAGARA JUKWAANI...
MBIO za kumsaka mrembo wa Tanga zimeanza! Jumla ya warembo 9 walipanda jukwaani kuchuana kuwania nafasi za kushiriki katika shindano la Miss Tanga kupitia kitogoji cha Miss Usagara, ambapo tano bora ya warembo hao watapata tiketi ya moja kwa moja kuingia katika fainali za Miss Tanga 2008.
Kitongoji hicho cha kwanza kufanyika Miss Usagara 2008, kimefanyika Mei 2 katika Ukumbi wa Splended Jijini hapa, ambapo mwanamuziki wa muziki wa kizazi kipya nchini anayetamba kwa sasa na wimbo wake Ni Soo!, Haji Mtepa al'maarufu kwa jina la Pasha ndiye aliyetifua vumbi usiku huo katika kinyang'anyiro hicho.
Onyesho hilo linaratibiwa na Lilian Kihama Maim kupitia kampuni yake ya Sunrise Secretarial & Beauty Saloon na limefanyika katika Ukumbi wa Splended Jijini hapa.
Warembo hao tisa walikuwa ni pamoja na Aisha Abdallah, Judith Asei, Hawa Njama, Amina Sadik, Khadija Ramadhani, Salma Mohamed, Merry Fedrick, Oliva Mango na Nuru Sheshe.
Judith Assey ndiye aliyetwaa taji la Miss Usagara 2008.

Mshindi wa pili kulia ni Oliver Mango na mshindi wa tatu kushoto ni Nuru Salim. Aliyevikwa taji la Mwenye kipaji kwa warembo wa Usagara ni Amina Sadick na taji la tabia njema lilikwenda kwa Hadija Ramadhani Kulia. Tano bora ya miss usagara inaingia moja kwa moja katika fainali za Miss Tanga 2008.
MIss Lushoto nayo hiyo..
